Monday, July 16, 2012

What makes the Unity of The Church

Katika nyakati za leo kanisa limekuwa mhanga mkubwa wa migawanyiko,migogoro na magomvi na kumbe sababu kubwa ni kanisa lenyewe"waamini" ndio wanaosababisha hayo!
Wanasababisha hayo kwa sababu...kanisa linaacha mambo ya msingi kama vile Imani moja,roho mmoja,ubatizo mmoja...na kushikilia vitu ambavyo si msingi ambavyo huleta migawanyiko.
Hayo yalisemwa na Pastor Matthew Sasali,alipokuwa akihudumu katika kanisa la TAG sayuni huko Isanga jijini Mbeya.
Alisema yapo mambo ambayo waamini wanatakiwa kuyaishi na hayo ndio ulinzi kwa kanisa...maana kanisa hushambuliwa sana na Adui kwa kuleta vitu vidogo vidogo ambavyo kama hawatakuwa makini...migawanyiko na malumbano havitaliacha kanisa.
Akitaja vitu hivyo Pastor Matthew alisema
1.Watu wanaacha mambo ya msingi yanatotuunganisha na kuweka mkazo kwenye vitu vidogo vya kututofautisha kama vile Haiba,Uwezo,Utashi....Mungu kama baba yetu alituumba tofauti na mara zote hufurahia tofauti zetu...na yeye anapenda tuwe na umoja na sisi tufanane...unity and not uniformity.
2.Lazima waamini wachague kutia moyo na si kukosoa kila jambo.
Ni rahisi kukaa pembeni na kunyoosha kidole cha kukosoa kwa mtu anayetenda jambo,ila ni ngumu sana mtu kuwa sehemu ya kutia oyo jambo linalotendwa.
 #kwa kukosoa mtu huaribu ushirika wake na Mungu
#kwa kukosoa mtu hufunua kiburi chake
#kwa kukosoa mtu hujiweka mahali pa yeye kuhukumiwa
#kwa kukosoa mtu husababisha maumivu katika kundi la Mungu.
3.Wengi hujua kuwa usengenyaji ni dhambi na huishia hapo...Pastor matthew akaendela kufundisha na kusema,lazima waamini wachague Kukataa kusikiliza Masengenyo
Kwa kukataa kusikiliza Umbeya kunaleta ulinzi ndani ya kaisa la Mungu ambalo leo hii limekuwa likisumbuliwa sana na Umbeya na masengenyo.
4.Ni muhimu waamini wakachagua Kumtia Moyo Mchungaji ama viongozi wa kanisa.
Hii inamaanisha uwepo umoja wenye kujenga kati ya Mchungaji na viongozi wa kanisa...kwani Mungu huweka maono ya mwelekeo wa kanisa kwa mchungaji na yeye atawajibika mbele za Mungu kwa ajili ya washirika wake...

No comments:

Post a Comment