Friday, June 22, 2012

Udadisi ni muhimu kwa maisha ya Leo

Ulimwengu uko hivi ulivyo leo kwa sababu miaka fulani huko nyuma watu wamewahi kuwa wadadisi...ambao ulipelekea kuwa na mambo mengi mazuri na makubwa ya hivi leo.
Udadisi ni hali inayompelekea mtu kuwa "genius" mwenye ufahamu mkubwa.Sidhani kama unaweza kukuta mwna taaluma mkubwa bila nyuma yake kuwa na Tabia ya Udadisi...
Hebu tuangalie kwa nini Udadisi ni kitu cha thamani...
1....Hufanya ufahamu kujishughulisha...kutokuwa na fikra Mgando.
Watu wadadisi mara zote huuliza maswali na hutafuta tafuta majibu ya maswali hayo katika fikra zao.Ufahamu wao mara zote hujishughulisha,na kwa kadri hufahamu unavyojishughulisha ni kama misuri ya kufikiri na kupata majibu nayo hutanuka...na kwa sababu huwa tabia na zoezi la mara kwa mara...basi ule uwezo wa akili unaosababishwa na udadisi hufanyika imara na fikra hukuzwa.
2....Hufanya ufahamu wako kufungua milango ya mawazo mapya
Kumbuka pale unapoanza udadisi juu ya kitu fulani...fahamu zako huweka matarajio na kuwa tayari kupokea mawazo mapya ya jambo lile.
Na pindi wako linapokuja fahamu hulitambua na kulikubali.Bila udadisi wazo jipya laweza kukupita na kujikuta ukikosa mambo mengi kwa sababu tu ufahamu haukutayarishwa kupokea....swali kwako...mawazo mangapi mazuri,mapya yamekupita kwa sababu tu ulikosa udadisi juu ya jambo fulani?
3....hukufungulia ulimwengu mpya na yanayowezekana
Kwa kuwa mdadisi unapata fursa ya kuona ulimwengu mpya na kuvuka na kukutana na mambo ambayo ulidhani hayawezekani hapo awali...vitu vyote huwezi kuona kama si kwa udadisi.Hayo yamefichwa chini ya maisha ya kawaida (yasio ya udadisi)inahitaji udadisi kufunua na kugundua ulimwengu mwingine ambao hukuwahi kuwa kabla na kugunduka kuwa yanawezekana.

4...hufanya maisha kuwa na mvuto.
Maisha ya Udadisi ni tofauti sana na maisha ya kawaida yaliyodumaa na yanayojirudia.Maisha ya udadisi mara zote yana mambo mapya ambayo huvutia "attraction" na huwashika watu "attention".

How to Translate your dreams into the reality.

Watu wengi tunaona maisha ni magumu...lakini si kweli,ila tu hatuna ndoto za baadaye za maisha yetu.Tumesahau kuwa maisha yetu ya baadaye yanaandaliwa na heka heka za leo...wengi hatuna focus/dream/purpose ya maisha yetu...Ni muhimu kuwa na Ndoto tena si ndoto tu Ndoto kubwa.
Na wengine wamekuwa na Ndoto nyingi tena nzuri...Tatizo linakuja namna ya kuifanya ndoto hiyo iwe halisia "reality"
Mch Matthew Sasali aliyasema hayo kwa wanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe tawi la Mbeya katika semina iliyoanza jana katika kuwaweka vizuri kwa habari ya maandalizi yao ya mitihani ya mwisho inayotarajiwa kuanza juma lijalo.
Pastor Matthew,aliweka hamasa kubwa ya kuwa na Ndoto ya maisha yao ya baadaye akitumia Mfano wa Yusufu katika kitabu cha mwanzo 37...ambaye aliona maisha yake miaka mingi ijayo.
Akiendelea kufundisha alisema yako mambo muhimu ambayo kila mwenye ndoto anatakiwa kuishi...ni kama mama mjamzito siku anapojigundua ana kitu tumboni mwake...kila kitu hubadilika na mfumo mzima wa maisha hubadilia ili kuhakikisha ndoto ya mtoto kuzaliwa inatimia.
Pastor akafundisha Vitu Kumi...kwa kupitia Neno "DEDICATION" herufi moja kwenda nyingine
Depend on Holy Spirit,Endure Hardships,Define your Focus,Internalization,Courage,Attitude(Descipline),Take Risk,Inspiration,Open your Mind(Exposure), na Never Give up.
Na mwisho kabisa Mch Matthew alipata fursa ya kuomba pamoja nao...Bwana awape Ndoto na kwa wengine...kutembea katika hayo...na kwa wote kwa ajili ya maandalizi ya mitihani yao.
Pastor Matthew ni Mchungaji,pia ni Meneja wa kituo cha Redio Ushindi Mbeya na sehemu kubwa ya huduma yake ni kwa wanafunzi wa vyuo.