Thursday, June 28, 2012

How to Respond to False Accusition

Mara nyingi watu wamekuwa wakikosea sana kujibu...pale wanapokabiliwa na tuhuma ama wamesingiziwa huku hawakufanya jambo lile..aidha kwa hasira ama kwa kutokujua basi hujikuta unajiingiza mtegoni na kujikuta huna namna ya kutoka kisha watu huthibitisha na kusema ulihusika ama ulifanya kweli...
Pastor Matt aliona ni vizuri akushirikishe namna hii ya kujibu pale unapokabiliwa na mashitaka ya uongo...ama ni kweli hukuhusika...

1.USISEME KITU...hii hutegemea sana hali ya tukio lenyewe lilivyofikia,lakini mara nyingi mtu akikutuhumu ni vyema ukanyamaza kwanza.Waweza kuona ni kama ni ushauri wa ajabu.Ukweli ni kwamba wakati huo kiwango cha hasira huwa juu.Unajua mpaka mtu anakutuhumu yeye mwenyewe anakuwa tayari amejichanganya ama yeye tayari ana hasira.Kuna nyakati tuhuma zinatakiwa kujibiwa papo hapo...ikiwa hivyo badilisha mtazamo kwanza.Kwa upole na busara ongea na mtu ambaye amekutuhumu na kumpa nafasi ya yeye kujieleza ili kujua ukweli,hii itakusaida wewe kujipanga...tena ukiweza fanya hili mara tu.
2.TAFUTA MSAADA...tayari umeshatuhumiwa...tafuta muda na uwe makini kutafuta msaada,waweza kuwa wa kisheria,ama mashauri tu au vinginevyo.Kama huna uhakika ongea na mwanasheria azungumze nao.Usidharau hatua hii tafadhali ni muhimu sana...mambo mengine huonekana ni madogo lakini muda mfupi baadaye huwa makubwa na huchanganya akili mno...na hujikuta unapoteza uwezo wako wa kutumia akili ipasavyo.
3.KUSANYA VIELELEZO...na kwa kuwa unajua wewe huna hatia,huo ni muda wako mzuri wa kukusanya vielelezo/ushahidi ili kueleza ukweli wa jambo lako.Hivi vyaweza kuwa vya namana mbali mbali....labda ni risiti,tiketi,kumbukumbu za benki,barua pepe n.k...jitahidi kupata vielelezo vya maandishi mara nyingi huwa msaada mzuri.
4.ANDAA NAMNA YA KUJIBU...chukua vielelezo vyako na uvipangilie vizuri ili vilete mantiki kwa mtiririko unaeleweka.Mpangilio ni ufunguo mzuri wa utetezi wako.Ukituhumiwa kwa maandishi jibu kwa maandishi.
5.FANYA MAWASILIANO NA MTU ALIYE KUTUHUMU...kama una mtu wa sheria anayekusaidia tfadhali fuata maelekezo.Tafuta muda wa kukutana na mhusika kisha ongea naye kuhusu hatua unazotaka kuchukua...kuna mawili mnaweza kujikuta unamaliza wenyewe...lakini unaweza ukajikuta unakwenda ngazi ya juu zaidi.
6.FAFANUA KWA UPANDE WAKO(JITETEE)...sasa uko uso kwa uso na aliyekutuhumu...ukitoa utetezi kuhusu tuhuma juu yako...1 kumbuka kuweka hisia kali mbali...kama ulijiandaa vizuri kwa hatua za mwanzoni utakuwa na kazi rahisi tu ya kuweka ukweli hadharani 2.weka vielelezo vyako kwa mpangilio 3.wape nafasi ya kujibu....wakati huo usitarajie wakuombe msamaha...laweza kuwa hivyo ama hapana.
Wakati huo wewe utakuwa umeweka kila kitu wazi...waamuzi wanauwezo wa kuona na kuamua.
 Nahisi kwa kuzingatia ya hapo juu wewe utakuwa salama....

Sunday, June 24, 2012

Principles of Receiving from God

Pastor Matthew Sasali akiongea na wanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe,Mbeya Campus juu ya kanuni muhimu ya mtu kupokea haja yake kutoka kwa Mungu,mwishoni wa wiki hili,hii ni katika kuhitimisha semina yake ya siku tatu chuoni hapo.Pastor Matt alitaja kanuni hizo ni
1.Kuna na Uelewa wa Kutosha juu ya Mungu unayemwomba
a.Omnipresent(yuko kila mahali) b.Omniscient(anajua yote) c.Omnipotent(mwenye nguvu zote)
2.Kwa kadri unavyomwelewa Mungu,ndivyo Imani yako kwa Mungu Huongezeka
3.Ni bora kuwa na Imani ndogo kwa Mungu mkubwa,kuliko Imani kubwa kwa Mungu Mdogo.
Pastor Matt aliyasema hayo na kufanya maombi nawanafunzi hao ili kuwaandaa na mitihani yao ya kumaliza mwaka.