Mch Matthew Sasali,ameeleza hayo leo katika ibada ya asubuhi katika kanisa la Rehoboth Internetional Christian centre,Forest Mpya jijini Mbeya,wakati akifundisha sifa za watu bora"wakuu" wa biblia na kutia shauku kwa wakristo wa leo kuambatana na sifa hizo ili wawe bora zaidi ya hao wa zamani wa biblia.
Pastor Matt alifundisha kuhusu watu tisa wakuu wa biblia na kuibua siri zilizowajenga hao,Huku akisema wakristo wa leo tunatakiwa kuwa na vigezo hivyo...
1.Imani kama ya Ibrahimu
2.Uongozi kama wa Musa
3.Ujasiri na Ushawishi kama wa Daniel
4.Bidii kama ya Paulo
5.Uaminifu kama wa Timotheo
6.Moyo wa toba kama wa Daudi
7.Hekima kama ya selemani
8.Uvumilivu na uadilifu kama wa Ayubu
9.Upendo na Huruma kama ya Yesu
Na baadaye katika ibada ya pili Mch Matthew alifundisha juu ya UTII UNAOLETA BARAKA kwa kutumia kitabu cha Luka sura ya 5 mstari wa kwanza mpaka wa kumi na moja juu ya hadithi ya Simon na nduguze baada ya kukutana na Yesu na kutakiwa kwenda kushusha nyavu zao kilindini
1.Alisema kuna nyakati tunaona kama Yesu hajishughulishi na maisha yetu...kumbe anatutazama na ili afanye kitu kwetu anahitaji utii wetu
2.Zipo nyakati ujuzi wetu katika maisha"experinces" waweza kuwa kikwazo kwa utii wetu kwa Mungu
3.Iwe tunaamini ama hatuamini,tunatakiwa kutii hapo ndio baraka zetu zilipo.
Matthew sasali ni Mch na Mwalimu wa Neno la Mungu,lakini pia ni meneja wa Redio Ushindi inayorusha mawimbi yake Nyanda za juu kusini,amemuoa Becky na amebarikiwa kuwa na watoto watatu NigEl,Nicola na Natasha.
Amen..nimepata kitu, barikiwa pastor!
ReplyDelete