Monday, June 11, 2012

What we Miss is Commitment

Siku ya jumapili ya tarehe 10/06/2012 Pastor matthew Sasali alikuwa Mgeni Rasmi kwenye Graduation ya wanafunzi wa Chuo kikuu Mzumbe(USCF-Mbeya Campus)na kupata nafasi ya kutoa changamoto kuhusu mambo ya kiroho,maisha ya kila siku na kisiasa pia.
Sherehe hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya,Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Mkuu wa chuo hicho Campus ya Mbeya...ambaye aliwaasa wanafunzi kufanya bidii,kujituma huku wakiepuka vishawishi ambavyo vinaweza kuwaharibia maisha yako na kupata magonjwa kama ukimwi.
Pastor Matt alieleza kuwa Taifa letu lina wasomi wengi,wataalam wa kila aina,rasirimali nyingi...ila limekosa watu walio COmmitted kwa ajili ya kuinua Taifa letu...aliendelea na kusema Commitment hujengwa tangu ndogo mpaka Kubwa hutokea...na kwa kizazi hiki huu ndio wakati wa kuanza kujenga Commitment...hivyo hupelekea mafanikio katika weledi wao pindi wanapoingia kazini.
 Pastor Matthew Alipata tena wasaa wa kuongea na wanafunzi hao juu ya siasa ya nchi yetu...na kuanza kujenga ushawishi wa kuwataka vijana hao wawe wa kwanza kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali kwani kilio kikubwa cha taifa letu ni kukosa viongozi waadilifu...Lakini kwa wao kugombea nafasi mbali mbali na kisha kupata nafasi hizo zinaleta mabadiliko,ustawi na uponyaji wa kwa Taifa letu kwa kuwa wao wana kitu cha Ziada nacho ni UCHAJI WA MUNGU.

Careful with Opportunities

Leo yamkini tusingekuwa hivi tulivyo kama tungetumia fursa fulani zilizowahi kujitokeza kwenye maisha yetu...yamkini tumebaki na majuto lakini hakuna namna ya kuziba.
Mara zote ukipoteza fursa fulani kwenye maisha huwezi kukwepa kuijutia.
Hayo yalisemwa na Pastor Matthew Sasali alipokuwa akiongea na wanachuo wa chuo cha MMTC Mbeya Medical Training Center kilichopo Hospital ya Rufaa Mkoani Mbeya,wakati wa sherehe za Graduation kwenye fellowship ya wapendwa chini ya mwamvuli wa TAFES.
Aliongeza na kusema,mara nyingi watu wamekuwa na kawaida ya kudharau mambo yanayowatokea huku wakidhani yatatokea tena...hivyo hawako makini hata kwa fursa ambazo kumbe hazirudii tena.
Kwa kuelezea akatoa mfano na kusema kama tungerudishwa nyuma na kuwa sekondari hivi tulivyo sasa,wengi wakasema tungefanya vizuri zaidi ya tulivyofanya wakati ule...sababu:wengi hawakujua kuwa muda ule na madarasa yale ni fursa ambayo ilitakiwa itumiwe vizuri na kujenga future nzuri baadaye.
 Mkazo mkubwa ilikuwa ni kuwa makini kwa Neno la Mungu ambalo huja kama nafasi adimu ili kutuinua...kuwa makini kwa watu ambao Mungu huwaleta kwenye maisha yetu...,matukio mbali mbali ambayo yamkini huwa kama ngekewa na hayarudii tena....Maana humo ndio kuliko na nafasi zetu za kutoka na kuchanua.Na mwisho kulikuwa na chakula cha Pamoja katika kufurahia miisho hiyo ya kuagana.
Mchungaji Matthew Sasali pia ni meneja wa Redio Ushindi Mbeya amekuwa na huduma kubwa kwa  wanafunzi wa vyuo akifundisha neno la Mungu na kujenga ushawishi na pia kuleta changamoto namna wanavyofikiri.