Monday, June 11, 2012

What we Miss is Commitment

Siku ya jumapili ya tarehe 10/06/2012 Pastor matthew Sasali alikuwa Mgeni Rasmi kwenye Graduation ya wanafunzi wa Chuo kikuu Mzumbe(USCF-Mbeya Campus)na kupata nafasi ya kutoa changamoto kuhusu mambo ya kiroho,maisha ya kila siku na kisiasa pia.
Sherehe hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya,Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Mkuu wa chuo hicho Campus ya Mbeya...ambaye aliwaasa wanafunzi kufanya bidii,kujituma huku wakiepuka vishawishi ambavyo vinaweza kuwaharibia maisha yako na kupata magonjwa kama ukimwi.
Pastor Matt alieleza kuwa Taifa letu lina wasomi wengi,wataalam wa kila aina,rasirimali nyingi...ila limekosa watu walio COmmitted kwa ajili ya kuinua Taifa letu...aliendelea na kusema Commitment hujengwa tangu ndogo mpaka Kubwa hutokea...na kwa kizazi hiki huu ndio wakati wa kuanza kujenga Commitment...hivyo hupelekea mafanikio katika weledi wao pindi wanapoingia kazini.
 Pastor Matthew Alipata tena wasaa wa kuongea na wanafunzi hao juu ya siasa ya nchi yetu...na kuanza kujenga ushawishi wa kuwataka vijana hao wawe wa kwanza kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali kwani kilio kikubwa cha taifa letu ni kukosa viongozi waadilifu...Lakini kwa wao kugombea nafasi mbali mbali na kisha kupata nafasi hizo zinaleta mabadiliko,ustawi na uponyaji wa kwa Taifa letu kwa kuwa wao wana kitu cha Ziada nacho ni UCHAJI WA MUNGU.

No comments:

Post a Comment