Friday, June 22, 2012

How to Translate your dreams into the reality.

Watu wengi tunaona maisha ni magumu...lakini si kweli,ila tu hatuna ndoto za baadaye za maisha yetu.Tumesahau kuwa maisha yetu ya baadaye yanaandaliwa na heka heka za leo...wengi hatuna focus/dream/purpose ya maisha yetu...Ni muhimu kuwa na Ndoto tena si ndoto tu Ndoto kubwa.
Na wengine wamekuwa na Ndoto nyingi tena nzuri...Tatizo linakuja namna ya kuifanya ndoto hiyo iwe halisia "reality"
Mch Matthew Sasali aliyasema hayo kwa wanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe tawi la Mbeya katika semina iliyoanza jana katika kuwaweka vizuri kwa habari ya maandalizi yao ya mitihani ya mwisho inayotarajiwa kuanza juma lijalo.
Pastor Matthew,aliweka hamasa kubwa ya kuwa na Ndoto ya maisha yao ya baadaye akitumia Mfano wa Yusufu katika kitabu cha mwanzo 37...ambaye aliona maisha yake miaka mingi ijayo.
Akiendelea kufundisha alisema yako mambo muhimu ambayo kila mwenye ndoto anatakiwa kuishi...ni kama mama mjamzito siku anapojigundua ana kitu tumboni mwake...kila kitu hubadilika na mfumo mzima wa maisha hubadilia ili kuhakikisha ndoto ya mtoto kuzaliwa inatimia.
Pastor akafundisha Vitu Kumi...kwa kupitia Neno "DEDICATION" herufi moja kwenda nyingine
Depend on Holy Spirit,Endure Hardships,Define your Focus,Internalization,Courage,Attitude(Descipline),Take Risk,Inspiration,Open your Mind(Exposure), na Never Give up.
Na mwisho kabisa Mch Matthew alipata fursa ya kuomba pamoja nao...Bwana awape Ndoto na kwa wengine...kutembea katika hayo...na kwa wote kwa ajili ya maandalizi ya mitihani yao.
Pastor Matthew ni Mchungaji,pia ni Meneja wa kituo cha Redio Ushindi Mbeya na sehemu kubwa ya huduma yake ni kwa wanafunzi wa vyuo.

No comments:

Post a Comment